Idara ya Uinjilisti na Umisheni
Habari njema kwa kila kiumbe
“Akawaambia, Enendeni ulimwenguni mwote, mkaihubiri Injili kwa kila kiumbe.”Marko 16:15
Tunawafikia watu kwa Neno la Mungu kupitia mikutano ya Injili, ushuhudiaji, vipeperushi na ufuatiliaji wa waongofu wapya.
Soma vipeperushi
Tunachofanya
Injili inawafikia watu
Idara huandaa mikutano na safari za Uinjilisti kwa kuwahudumia watu kwa Neno, maombi na upendo.



Ripoti ya Uinjilisti 2025
Mavuno katika maeneo tuliyofikia
Mwenge Gospel Runners ilihubiri Injili katika mikutano minane iliyofanyika Tabora, Singida na Tanga. Takwimu hizi zimetokana na ripoti ya Idara ya Uinjilisti ya mwaka 2025.
Bofya mkoa kuona taarifa za uinjilisti
Tabora
Mwakashanhara 38 · Puge 21
Singida
Ibaga 26 · Ilongelo 16
Tanga
Gharambo 114 · Mkuzi 33 · Kwamba 38 · Tunguli 40
Idadi inaonyesha watu walioamua kumpokea Kristo katika kila eneo. Hatua inayofuata ni kuimarisha malezi na ufuatiliaji wa kila mwongofu mpya.
Mikoa yote ya Tanzania
Chagua mkoa
Mikoa yenye ripoti itaonyesha maeneo na idadi; mingine itaandikwa “Itakuja hivi punde.”
Maktaba ya Uinjilisti
Vipeperushi vya Uinjilisti
Chagua kipeperushi unachotaka kusoma. Unaweza kukifungua hapa au kukipakua kwa matumizi ya Uinjilisti.
Mapambano
Kipeperushi cha mafundisho ya kiroho.
Mapambano ya Katuni
Kipeperushi chenye kurasa za mbele na nyuma.
Kizuizi Kimeondolewa
Ujumbe wa tumaini na wokovu.
Utamlaumu Nani?
Kipeperushi cha Injili na mwito wa kufanya uamuzi.
Kipeperushi cha Watoto
Ujumbe wa Injili ulioandaliwa kwa ajili ya watoto.
Malezi na ufuatiliaji
Fomu ya mwongofu mpya
Sajili taarifa za msingi kwa usahihi ili timu ya malezi iweze kumpokea, kumfuatilia na kumsaidia mwongofu mpya kukua ndani ya Kristo. Taarifa hizi ni za matumizi ya ndani ya kanisa pekee.



